Wednesday 30 September 2015

JIFUNZE NAMNA YA KUFANYA MANUNUZI EBAY

Ebay ni sehemu ambayo wauzaji na wanunuaji  wanakutana
Muuzaji  anajiunga kwa kufungua Account ebay na kisha anatangaza kitu anachokiuza akiwa popote pale Duniani
Mnunuzi anajiunga kwa kufungua Account ebay popote alipo Duniani kisha anachagua bidhaa anayoitaka iliyotangazwa na Muuzaji(Seller) ana inunua online.




 MAMBO YA KUZINGATIA ILI KUTUMIA EBAY

1. Tafuta Debit card au Credit card

Debit card ni kadi inayokuwezesha kununua vitu kwenye mtandao kwa kutumia pesa iliyo kwenye akaunti yako ya benki. Na Credit card inakuwezesha kununua kwa kukopa kwenye benki unayotumia halafu wanakukata kidogokidgo kwenye mshahara wako au namna yoyote ambayo mtakubaliana na benki. Kadi hizi ni kama Tembo card visa na Tembo card master card za CRDB Bank;

benki zingine kama NBC, Stanbic Bank na BARCLAYS Bank pia zinatoa Kadi Za namna hiyo. Baada ya kupata kadi yako unatakiwa uende kwenye benki yako wakairuhusu kuweza kufanya manunuzi kwenye mtandao.

2. Jiunge na tovuti ya Paypal.

Paypal ni tovuti inayoongoza duniani kwa kusimia malipo ya kwenye mtandao. Kazi yake kubwa ni kutunza taarifa zako muhimu za benki ili wamachinga wa kwenye mtandao wasizizoee hovyo. Hivyo basi ukitumia paypal, unasajili na kuweka namba yako ya visa au master card.

Baada ya hapo unaweza kuweka pesa kwenye account ya paypal au ukaziacha kwenye akaunti yako ya benki. Unapofanya manunuzi Yule muuzaji anapewa pesa na Paypal sio wewe moja kwa moja ili kulinda taarifa zako za benki.

3. Nunua kwenye tovuti iliyo na mfumo wa kutuma taarifa zako kwa usalama.


Kwa ajili ya usalama kuna teknologia inaitwa SSL(Secure Socket Layer). SSL inafanya kazi ya kusafirisha taarifa zako katika hali ya mkanganyiko ili mtu yoyote mhalifu asiweze kuzielewa, zikifika zianaundwa tena ili muuzaji aweze kuzielewa.

Teknologia hii inatumika pia kutuma email, blackberry wakiwa ni vinara wa kutunia teknologia hii. Ili kujua kama tovuti inatumia hii teknologia utaona alama ya kufuli kwenye anuani ya tovuti husika ikishafunguka. Angalia kwenye sehemu ya kuandikia anuani, kushoto au kulia.

4. Nunua kwa muuzaji anayekubaliwa na weteja wengi.

Utajuaje kama muuzaji anakubalika sokoni na anauzoefu wa kuuza vitu kwenye mtandao? Rahisi! Kwa mfanounataka kununua saa Ebay au kitabu cha electrniki (PDF) kwenye Amazon, chini ya hiyo bidhaa iliyoichagua utaona maoni ya watu walionunua kabla yako.

Ni vizuri ukatumia muda wa kutosha kusoma maoni ya waru wengi kabla hujaendelea za zoezi la manunuzi. Njia nyingine ya kupata maoni ya watu ni kutumia tovuti kama Yelp, Google+, Yahoo directory au Yellow pages iwapo muuazaji atakuwa amejiunga nazo.

5. Chagua namna ya kutumiwa mzigo wako.

Unatakiwa kuchagua namna kutumiwa mzigo wako ambayo itakuwa rahisi kwako kuupata. Gharama za kutuma mzigo zitaoneshwa pale kwenye mtandao na muda wa kufika kwa kila gharama. Kwa Tanzania unaweza kutumia DHL, UPS au shirika lolote unaloliamini.

6. Hakikisha muuzaji anahudumia eneo ulilopo.

Baadi ya wauzaji huchagua nchi au miji wanayoweza kutuma mizigo na wengine huuza dunia nzima. Taarifa hizi huwekwa chini ya bidhaa unayotaka kununua , hii itakusaidia kuokoa muda kuondoa usumbufu usio wa lazima.
 


   

Pia waweza tumia njia hizo kwa mitandao mengine tofauti na ebay ila zingatia:
Unaponunua kitu kwenye mtandao kwanza kabisa hakikisha hiyo tovuti inafahamika, kama haifahamiki hakikisha kuwa imethibishwa na na mashirika yakuhalalisha biashara za kwenye mtandao kama BBB (Better Business Bureau), utaona nembo ya haya mashirika chini kwenye tovuti ya muuzaji.


 kwa mungozo zaiidi na maswali bonyeza hapa

Share:

0 comments:

Post a Comment

nature beauty

Powered by Blogger.

recent posts

Total Pageviews

Search This Blog

technology

Number of Posts

featured video

Random Post Number

Slider Display

Random

The Slider

social counter

twocolumns

about us

About

Formulir Kontak

Name

Email *

Message *

Social Icons

Featured Posts

FOLLOW @ INSTAGRAM

Must read