Sunday 2 July 2017
Monday 23 May 2016
Fahamu namna ya kutumia whatsapp account mbli katika simu yako
Je umesha wahi kutamani kutumia social network account zaidi ya moja katika smartphone yako ...!!!! . Sasa unaweza kuwa na account zaidi ya moja ,waweza kuwa na social network account mbili,kama vile whatsapp, facebook,twitter,Instagram,snapchat , katika simu yako moja na kuzitumia kwa wakati mmoja kwa kutumia
'Parrallel space app' app hii itakuwezesha kutimiza lengo lako
Waweza kuidownload Parrellel space app hii bonyeza hapa ukisha download hii utaweza kuadd any social network account unayo hitaji pia waweza kuadd online game account zaidi ya moja
Tuesday 12 January 2016
JINSI YA KUANGALIA SIMU KAMA NI FEKI
Makala hii itakuonesha jinsi ya kuangalia kama simu yako ni feki ama la.
Zifuatazo ni hatua unazoweza kuzitumia kuangalia kama simu yako ni feki, hakuna mahitaji makubwa kufanya hili ila tu unahitaji simu yako unayoitumia na unayotaka kuiangalia.
Jinsi ya angalia IMEI namba
Andika *#06# kisha bonyeza kitufe cha kupiga
Baada ya hapo simu yako itakuletea IMEI namba ambapo kama simu yako au kifaa chako kina laini mbili basi kutakuwa na IMEI namba mbili
Namba hii pia unaweza kuipata katika boksi la simu ama nyuma ya ya simu hiyo baada ya kutoa betri, utaijua kwa kuwa huwa ni tarakimu 15.
Nakili namba hizo pembeni.
Jinsi ya kuangalia kifaa kama ni feki ama halali
Iandike ile namba uliyo nakili katika hatua iliyopita katika sehemu ya kuandikia ujumbe
(SMS)
Utume ujumbe huo kwenda namba 15090
Baada ya kutuma meseji hiyo utaangaliziwa je hiyo IMEI namba ni ya simu ya aina gani na nani mtengenezaji wa simu hiyo.
Subiri majibu (haitachukua muda mrefu)
Ujumbe huo ukija unakuwa na maelezo ya kampuni iliyotengeneza simu hiyo pamoja na jina la simu hiyo.
jinsi ya kuaangalia simu kama feki Mfano wa ujumbe unarudishwa baada ya kutuma IMEI namba
Jinsi ya kujua kama simu yako ni feki
Kama jina la mtengenezaji wa simu yako pamoja na aina ya simu yako (Uliyo jibiwa baada ya kutuma IMEI namba) haviendani na majina ya simu yako (ambayo yameandikwa katika simu yako) basi ujue simu yako inamashaka na ni vyema kumuuliza muuzaji wako juu ya hilo.
Kama majina yaliyorudi hayaendani na majina yaliyoandikwa katika simu yako basi upo katika kundi lenye uwezekano wa kuwa na matatizo, TUNAKUSHAURI ufuate utaratibu na kuibadilisha ama kuacha kuitumia simu hiyo kabla ya mwezi Juni.
Kwanini TCRA wanataka tubadilishe simu
Simu isiyo na IMEI ni sawa na gari lisilo na namba za usajili {plate number}
Vyombo vya usalama vinaweza kukamata wahalifu wa kutumia mitandao ya simu kwa msaada wa IMEI namba hivyo mtu akiwa anatumia simu ambayo haina au ina IMEI namba ambayo sio sahihi anazuia utendaji kazi wa taasisi za usalama hivyo wao kama mamlaka wanatakiwa kuhakikisha kila mtu anatumia simu yenye IMEI namba sahihi.
Saturday 9 January 2016
Ifahamu simu janja yenye uwezo wa kukaa na chaji zaidi ya siku kumi
Simu janja yenye uwezo wa kukaa na chaji kwa zaidi ya siku 10? Haraka haraka jambo hili linaonekana bado ni ndoto ila tayari kuna kampuni ambayo imedai imefanikisha jambo hili na simu zake zitaanza kupatikana mapema mwezi wa kwanza, 2016.
Simu janja hiyo inakuja na betri lenye kiwango kikubwa cha uhifadhi chaji wa mAh 10,000 italetwa na kampuni iitwayo Oukitel. Wenyewe wanasema kwa matumizi ya ‘kawaida’ wanategemea simu hiyo iweze kukaa na chaji kwa zaidi ya siku 10, wanasema kutegemea na utumiaji inaweza fikisha hadi siku 15.
Oukitel K10000Oukitel K10000
Kampuni hiyo tayari miezi kadhaa nyuma ilishawahi kutoa simu janja yenye kiwango kikubwa cha uhifadhi chaji wa mAh 6000.
Simu hii ya kiwango cha chaji cha mAh 10,000 itachukua jina la Oukitel K10000 na inakuja ikitumia toleo la Android 5,1 Lollipop.
Kupitia simu hiyo utaweza pia kuitumia kama vile ‘powerbank’ ili kuweza kuchaji simu yako nyingine ya ziada. :-)
Sifa zinginezo za Oukitel K10000
Kioo (display) ya Inchi 5.5 HD (720X1280)
Prosesa – 1GHz quad-core MediaTek MT6735
RAM GB 2
Diski Uhifadhi (Storage) – GB 16 na uwezo wa kutumia kadi ya microSD
Kamera ya mbele ya MegaPixel 8 na ya selfi MegaPixel 2
Kamera ya mbele inakuja na teknolojia za HDR, kutambua sura (face detection), uwezo wa kupiga picha za panorama n.k
Kimawasiliano inakuja na teknolojia za GPRS/EDGE na 3G, pia Bluetooth na WiFi.
Kwa sasa simu hiyo ishaanza kuuzwa kupitia mtandao wa GearBest kwa takribani dola 240 za Marekani, wanaolipia kwa sasa wataanza kuipata simu hiyo mwezi wa kwanza ambapo ndio pia itaanza kupatikana katika nchi zingine.
Monday 19 October 2015
ZIFAHAMU MONITORS NA DISPLAYS 10 BORA KWA SASA
Saturday 17 October 2015
LEO KATIKA TEKNOLOJIA ZIFAHAMU APPS ZILIZOINGIA KATIKA APPSAFRICAN INNOVATION AWARDS 2015
1. Best disruptive innovation
MicroEnsure (UK), Esoko (Ghana), Talking Bookz (Nigeria), Picup – South Africa, Opera’s Sponsored Web Pass – Nigeria
2. Best mobile innovation
Mobu – (Kenya), Chura – (Kenya), bookly – (South Africa), Ninayo – (Tanzania), M-vendr – (UK), ShoOwer – Cameroon
3. Best non data mobile innovation
TTC Mobile – (Uganda and Tanzania), Unotify (Rwanda), Totohealth (Kenya), GeoPoll (US and Kenya), SaferMom (Nigeria)
4. Best African app
Cross Dakar City (Senegal), bookly – (South Africa), Truppr (Nigeria), mPaper (Tanzania) and Tuluntulu (South Africa)
5. Best fintech innovation
Mergims (Rwanda), LipaPlus (Kenya) , SimbaPay (UK) ,VCpay (South Africa) , Mastercard/ Standard Bank MasterPass app (South Africa) and Verifone Mobile Money (Kenya)
6. Best health innovation
MOBicure (Nigeria), GiftedMom (Cameroon), Telemedicine Africa (South Africa), emocha Mobile Health (USA) and The Medical Concierge Group (Uganda)
7. Best educational innovation
mPaper (Tanzania), Flippy Campus (Ghana/Nigeria), bookly – (South Africa), SYNA (Nigeria) , Xander Apps (South Africa) and Bambisa (South Africa)
8. Social impact award
codeX (South Africa), bookly – (South Africa), 1task1job (Cameroon), UjuziKilimo (Kenya), and Afrikstart (UK).
9. Best entertainment innovation
Bozza Mobile (South Africa), GAMSOLE – Nigeria, MyMusic (Nigeria), Guumzo (Tanzania) and Media24 HYD 3D (South Africa)
10. Women in tech award
Emefa Kpegba (OMobileFunding – Togo), Anike Lawal (Mamalette -Nigeria), Linet Kwamboka (DataScience – Kenya), Zimba Women (Uganda) and Kelechi Anyadiegwu (Zuvaa -USA/Nigeria)